Total Pageviews

Friday, December 2, 2011

MY 21 DAYS VACATION TO NAKATUBA - KANISANI KIBARA

Jumamosi 15.10.2011, Sabato. Na safari mapema alfajiri ikianzia Kibara kumchukua Mama Tereza, kumleta Nakatuba kuteta na Dadie kabla ya safari ndefu jumapili, na baadae kurudi kushiriki sabato kanisani Kibara. Njiani nikavutiwa na taswira hii ya "Sunrise" nikiwa pale kilima cha Manana, jua likitoka usawa wa kilima cha Mmagunga
Baadae ikawa nafasi njema ya kushiriki Sabato katika kanisa la Kibara, Na kupata NENO kupitia kwa Mch Kamoga.
Miaka mingi iliyopita niliposali hapa kwa mara ya mwisho nililiona kanisa hili kuwa kubwa. Lakini sivyo ilivyo leo. Haliwezi tena kutosheleza na hivyo tunalazimika kufanya ibada nje ya kanisa.

Kanisa lina mpango mzuri ambao naamini Mungu ataubariki wa kujenga kanisa lingine kwa gharama ya Tshs Million Mia mbili.
Sehemu ya sadaka yetu itaenda kugharamia ujenzi huu
Mwongozaji wa kwaya, Mafuru Mafwili akiwajibika katika kinanda

Kwaya yenye talanta ya uimbaji haswa

Wakati wa kutoka nikapata nafasi ya kutambulishwa kwa ndugu na jamaa mbalimbali ambao hatujaonana miaka mingi, miongoni mwao Mke wa Uncle Kasina
Na Mama Makuke

No comments:

Post a Comment