Total Pageviews

Tuesday, June 25, 2013

GET WELL SOON MADIBA

Local and International Journalists wait outside the Pretoria hospital where former president Nelson Mandela is being treated.
Photo: Christa Van Der Walt/EWW

JELA

Ujumbe wa leo toka Daladala
"Kama Jela ni kuzuri, Mpeleke mwanao....."

Monday, June 24, 2013

UKISTAAJABU YA MUSSA............(Copy from Matukio - Michuzi)



MWANAMKE mkazi wa kijiji cha Ikandamoyo, wilayani Katavi, Veronica Saleh ‘Mama Kaela’ (50), amefanya uamuzi adimu wa kuolewa na wanaume wawili ambao anaishi nao kijijini hapo.

Kijiji hicho kipo umbali wa takribani kilometa 30 kutoka mjini hapa katika Jimbo la Katavi linalowakilishwa na Waziri Mkuu Mizengo Pinda.

Pamoja na ndoa hiyo iliyowezeshwa na mume mkubwa kukubali kuishi na mume mdogo, imeelezwa kuwa mwanamke huyo ndiye ‘aliyewaoa’ wanaume hao kwa zaidi ya miaka saba sasa, huku akiwa na amri kuu katika nyumba, kama ilivyo katika ndoa za kawaida.

Wanaume hao ni Paulo Sabuni ‘Baba Kaela’ (60) ambaye ndiye mume mkubwa na Arcado Mlele (45) ambaye ni mume mdogo.

Taarifa za kuwapo kwa ndoa hiyo ya aina yake, ziliifikia Globu ya Jamii na kufanyiwa uchunguzi kwa zaidi ya wiki tatu, na hatimaye katikati ya wiki hii, wahusika walikubali wao wenyewe kuzungumzia suala hilo. Kwa mujibu wa maelezo ya mwanamke huyo ambaye alionekana kuwa msemaji wa familia hiyo, yeye na mumewe mkubwa, walifika kijijini hapo miaka 24 iliyopita, wakitoka kijiji cha Usumbwa mpakani mwa Chunya, Mbeya na Tabora.

Wakiwa kijijini hapo mume wake aliendelea kufanya kazi ya ukulima wakati yeye mama (Veronica), pamoja na kilimo hujihusisha na upishi na uuzaji wa pombe ya kienyeji iitwayo kayoga.

Mwanamke huyo ambaye amesema ana watoto wanne, Alfred (20), binti mwenye miaka 16 (ambaye ameolewa) na wengine wawili wa kiume, mmoja akisoma darasa la sita na mdogo ana miaka saba, amesema hana shida na waume wake.

Ingawa wanandoa hao walizungumza kwa hadhari, majirani walikiri kuwa mwanamke huyo anaishi na wanaume hao wawili kwa amani na kwamba mwanamke huyo ndiye mwenye sauti na si waume zake.

“Si siri tena sasa, tumeshawazoea, kwani wanaishi kwa amani ila yule mume mdogo anaishi kwenye nyumba aliyoachiwa na marehemu baba yake, lakini anashinda kwa mume mkubwa, ambapo inajulikana kijijini hapa kuwa ni nyumba kubwa. “Basi pale ni mambo yote, kula na kunywa, mama huyu amewapangia zamu wanaume hao kama afanyavyo mume mwenye wake wengi. 

Ama kweli ukistaajabu ya Musa utaona ya Firauni,” alisema mkazi mmoja kwa masharti ya jina lake kutoandikwa gazetini. Ilielezwa, kwamba wanaume hao wana akili timamu na hawatumii kilevi cha pombe kama ilivyo kwa mke wao.

Hata hivyo, mume mkubwa anapewa sifa za upole tofauti na mume mdogo anayetajwa kuwa mkorofi kiasi cha mara kadhaa kumchapa makofi mkewe anapomuudhi.

Majirani wanadai kwamba Mama Kaela na mumewe Paulo, walipofika kijijini hapo, walipokewa na kuishi maisha ya kawaida, lakini baadaye mama huyo alianza kuwa na uhusiano wa kimapenzi na Arcado, ambaye naye alilazimika kuachana na mkewe wa ndoa anayefahamika kijijini hapo kwa jina la Mama Pere.

Ilielezwa na mashuhuda hao kwamba mume mkubwa alipobaini uhusiano huo, alikuja juu, lakini mwanamke huyo inadaiwa alimweleza mumewe huyo, atake asitake lazima wataishi wawili, vinginevyo ataachana naye, ndipo mume mkubwa alipokubali kuishi na mume mwenza.

Katika maisha ya kawaida katika familia hiyo, inaelezwa kwamba katika baadhi ya siku ikitokea kuwa mama huyo amechoka kupika, mume mdogo huchukua jukumu la kupika na kumwandalia chakula na maji ya kuoga mume mkubwa.

“Lakini mara nyingi kwa mfano, ikiwa ni zamu ya mama huyo kulala kwa mumewe mkubwa, basi humfulia nguo zake kisha anakwenda kwa mumewe mdogo nako anamfulia nguo.

“Ndivyo wanavyoishi, nasi sasa tumewazoea ila yule mama ni mkali na ana sauti pale kwake kwa wanaume wale ila tunaona kama ana wivu sana kwa huyu mdogo ambaye naye pia ana wivu kwa mkewe huyo, labda anahofia kuwa mama huyo anaweza kuongeza mwanamume mwingine,” anasema mmoja wa majirani hao.

Hakuna mazuri yasiyokuwa na machungu, japo familia hiyo inaelezwa kuwa na amani, mtoto wao mdogo nusura avuruge uhusiano wa wanandoa hao, baada ya kuibuka mzozo wakati wa maandalizi ya ubatizo wake.

Kwa sababu anazojua mama, ingawa inafahamika kuwa wote ni watoto wa mume mkubwa, mke huyo katika hati za ubatizo aliandikisha ubini wa mtoto huyo kuwa ni Mlele (akimaanisha kuwa mtoto wa mume mdogo), lakini mume mkubwa aliweka pingamizi kanisani akidai yeye ndiye baba halali wa mtoto huyo.

Kwa mujibu wa mwanamke huyo, yeye na Arcado ni waumini wa madhehebu ya Katoliki wakati Paulo ni Mpentekoste. Madai ya mzozo wa uhalali wa `ubaba’ wa mtoto huyo, yalithibitishwa na baadhi ya wakazi wa kijiji hicho, akiwamo mwalimu wa dini wa Kigango cha Kanisa Katoliki Uruira, Mashaka Abel. Walisema miaka sita iliyopita, mtoto huyo akiwa na umri wa mwaka mmoja, alifanyiwa taratibu za ubatizo, lakini ilishindikana, kutokana na wanaume hao, kila mmoja kudai ndiye baba mzazi wa mtoto.

“Lilikuwa jambo la kustaajabisha sana, kwani familia hiyo ilifanya maandalizi yote ya sherehe ya ubatizo wa mtoto huyo, lakini siku hiyo kanisani wakati huo ilikuwa ni kigango cha Katumba ambacho sasa ni Uruira, sakata lilianzia pale Padri alipomwuliza mama wa mtoto huyo ubini wa mtoto naye akasema ni Mlele.

“Hapo ndipo mume mkubwa alipopinga na kudai kuwa mtoto yule si wa Arcado bali wake na yeye ndiye baba halali. Padri hakuamini, aliuliza tena na tena na majibu yakawa ni yale yale, ndipo ubatizo ukashindikana,” alisema Katekista Abel.

Kazi ya kutafuta undani wa ndoa hiyo haikuwa rahisi kutokana na mazingira ya woga na usiri uliokusudiwa kubaki, ambapo awali mama alisema kwamba mume wake ni Paulo pekee japo siku ambayo mwandishi wa habari hizi alifika kijijini hapo na baadaye nyumbani kwa wanandoa hao na kumkuta mume mdogo (Arcado akimsaidia mkewe kukoroga pombe. Awali katika utambulisho, walidai kuwa ni mtu na mdogo wake na kusita kuzungumzia maisha yao ya kifamilia.

Mke wao ambaye alionekana wazi kuwa ni msemaji mkuu alifoka na kuja juu, akidai kuwa hayuko tayari kuzungumzia uhusiano wake na wanaume hao wawili, ingawa alikiri kuwa wanaishi pamoja.

"Kwa hiyo umefunga safari yote hii kutoka huko ulikotoka ili uje kwangu mie Veronica … nasema sitaki kabisa mtu kuja hapa na kutaka kunivurugia mpangilio wa maisha yangu, kwanza nani alikueleza hayo, wambea wakubwa hao yanawahusu nini watu hao?” alihoji.

“Mie mume wangu ni huyu Paulo basi … sasa leo umeniachia vurugu ndani ya nyumba nitapigwa na huyo mume wangu Paulo, kwani mmenishikisha ugoni?” alifoka Mama Kaela. Hata hivyo, mume mkubwa alidai kuwa hatamwadhibu mkewe huyo na kwamba wataendelea kuishi pamoja na mdogo wake Arcado kwa amani. Hata hivyo, akina mama wengi kijijini hapo wanalaani kitendo cha mama huyo kuishi na wanaume wawili ambapo waliomba uongozi wa Kanisa uingilie kati, ili mama huyo aweze kufunga ndoa na mume mmoja.

Lakini kwa upande mwingine, baadhi walimpongeza mwanamke huyo wakidai kuwa kitendo hicho ni cha kijasiri kwa mwanamke, kumudu kuishi na wanaume wawili na kuwa na mamlaka juu yao.


KWETU JUMAPILI

Wengine hutafuta habari, au kucheza game
 
Wengine ni wasusi
Na vinyozi pia tunao

Sunday, June 23, 2013

The GRANDs

 Billy
 Milly
 
Ukiona hivi, ujue Uzee umeshafika

TAKE 5

Kula Tano

LULU - KIKAO CHA SITA

 
 
Jumamosi 22.06.2013
Kama kawaida tumeendelea na kikao cha Sita cha maandalizi ya send Off ya Lulu Bhituro Bright.
Wadau wanazidi kutuunga mkono kwa siku chache zilizobakia.
Almost a dozen days to go.

Friday, June 21, 2013

WOMAN

Genesis 2:22

GET TO KNOW TANZANIA'S TOP RICHEST!!!

Said Salim Bakhresa
Net Worth: $620 million
Source: Manufacturing
Unarguably Tanzania’s richest man, Bakhresa dropped out of school at the age of 14 to launch his own business. He started out selling potato mix and subsequently opened a small restaurant in Dar es Salaam in the 1970s. As the restaurant operation expanded, Bakhresa used his profits to found a grain milling and food production company which formed the flagship for the Bakhresa group, a multinational manufacturing conglomerate which manufactures everything from maize flour and confectionaries to chocolates, ice cream, soft drinks and paper bags. Annual sales: $800 million. The group has manufacturing operations in Tanzania, Uganda, Malawi, Rwanda and Mozambique and employs over 2,000 people.Na sifa kubwa ya Bakhresa anajua sana kuwatake care stuff wake kwa kuwajali,,
Gulam Dewji
Net Worth: $560 million
Source: Manufacturing
Reclusive tycoon started out in the 70s importing key commodities into Tanzania. He grew the small trading operation into Mohammed Enterprises Tanzania, one of East Africa’s largest conglomerates. Key assets include 21st Century Textiles, one of the largest textile producers in Sub-Saharan Africa. The company’s four textile mills in Tanzania and Mozambique produce 100 million running meters of fabric annually. The group also manufactures Pride, Tanzania’s leading fruit beverage and everything from edible oils, toilet soaps, and artificial sweeteners to bicycles and motorcycles. The group also owns an insurance firm, container depots, a petroleum marketing company, a logistics outfit and a retail concern with over 100 outlets across Tanzania. Gulam’s son, Mohammed is a Member of Parliament in the National Assembly of Tanzania..
Rostam Aziz
Net worth: $420 million
Source: Telecoms, Mining, Shipping
A politician and businessman of Middle East origin, Rostam Aziz is one of Tanzania’s richest men. He was elected into parliament in 1993 and went on to win 2 consecutive terms as an MP. He quit politics in 2011 to focus exclusively on his businesses. Aziz’s family businesses include a 19 percent stake in Vodacom Tanzania, the country’s leading cellular network with over 8 million subscribers, Caspian – the country’s largest contract mining company and the Dar es Salaam Port which it owns in partnership with Hong Kong conglomerate Hutschison Whampoa.

.
Reginald Mengi
Net worth: $280 million
Source: Media, Coca-Cola Bottling, Gold Mining Mengi, a trained Chartered accountant is one of Africa’s most revered media moguls, and one of Tanzania’s wealthiest men. After practicing accounting, he ventured into private business by manufacturing and assembling ballpoint pens and selling to large retailers. Today, the IPP Group which he founded and chairs, owns 10 national newspapers (including Tanzania’s Financial Times, ThisDay and The Guardian), two of East Africa’s most popular Television stations (EATV and ITV), and about ten radio stations. He also owns a Coca-Cola bottling plant in Dar-es Salaam as well as two gold mining companies, IPP Gold and Handeni Gold in Tanzania.

Ali Mufuruki
Net worth: $110 million
Source: Retailing, Venture capital
Mufuruki is the founder and Executive chairman of Tanzania’s Infotech Investment Group. The group holds the Tanzanian and Ugandan franchise for South African retail giant Woolsworth. Infotech also has interests in property development and leasing, hospitality, advertising and mobile telecommunications. Mufuruki is also a co-founder and partner at East Africa Capital Partners, a technology, media and telecommunications sector focused Venture Capital Fund Manager investing in the greater Eastern Africa region. Also a prominent board room guru, Mufuruki sits on the boards of the Nation media group, East Africa’s largest media conglomerate and Stanbic bank Tanzania. He is also the chairman of Africa Leadership Initiative East Africa Foundation which aims to develop a new generation of values-based community spirited leaders in africa.
Source:http://darslamproductions.blogspot.com

Thursday, June 20, 2013

CAPTURING OF THE BLOGGER

 
Mambo ya kuutafuta mchana
Kawawa Rd, Msimbazi Centre/Lamada Hotels

UPENDO

Msisitizo wa Upendo

GREETINGS FROM FINLAND

 
pics from mtwara taken in front of house by finnish volunteers who lived with us, leena and taina,
bright

"Shikamoo! 
Habari ya familia Msalya? Habari ya Mtwara? Nimemisi Tansania. Habari ya finland ni nzuri sana. Haraka kidogo, kama kawaida lakini.

I promised to send you some pictures and I forgot all about it, I am sorry. But I will attach some pistures to this email. Hope you will enjoy them. Can you please say hello for everyone. I miss you all. Can you also say my greetings and best wishes to Bibi. I miss her so much.

With love,
Leena
"