Total Pageviews

Wednesday, November 9, 2011

MY 21 DAYS VACATION TO NAKATUBA - MSALYA TRACES

"MSALYA" Chisaka Maseme 1895 - 04 June 1966
Nimekuwa nikimfikiria mwanaume huyu wa shoka.
Hebu fikiria enzi hizo, kwa mikono yake mwenyewe.
Akachimbwa "Bwawa" la maji kwa matumizi ya familia yake tu.
Na miaka 45 baada ya kifo chake, na zaidi ya miaka 60 tokea alipoifanya shughuli hiyo.
Masalia ya kisima hiki yangalipo
Vacation yangu ilinifikisha kushuhudia tena kisima hiki.
Kuna alama nyingine muhimu aliyoileta Nakatuba.
mti huu, nimezaliwa nikiukuta
Na ungalipo leo ukizidi kuchanua.
Inasemekana Msalya alikuwa mtu wa masafa, na aina hii ya mti aliitoa mbali. lakini nikiri sijapata kuuona huu mmea zaidi ya Nakatuba.
Sidhani hata kama una jina la asili ya sehemu hii, kwani imebakia kujulikana kama "LIMEYA"
Miti mingine aliyoileta, ikijulikana kama "AMANAJI" ilishindwa kuvumilia ukatili wa wana Nakatuba, imetoweka ikifuata njia ya miti mingi mingineyo ya asili ya "AMAGOME", "JISUNGWA", JIFWITANDA", JISYEKA", na kadhalika
Mti huu inasemekana aliupanda au aliutunza wakati wa shughuli ya uchimbaji kisima.
"LIGOTOMELWA", umeendelea kuhimili mpaka sasa.
Ungekuwa unaweza kuandika historia, nadhani una mengi ya kusema uliyoyaona kwa watu waliokuwa wakioga chini yake kwa zaidi ya miaka hamsini iliyopita.
Sasa hivi tuna wataalamu wengi, labda siku moja kuna atakaeweza kuchora angalau kunipa picha ya Bw Msalya alivyokuwa akionekana.
Nina hakika vionjo vya sura yake havitakosekana ndani ya sura hizi
"TATU MAFURU"
"NYABHUTACHE MAPIGANO"
"Bintiye CHAUSIKU MSALYA"
Mwanae KULWIJIRA "CK" MSALYA"

Mwanae "MTESIGWA MWAYAI MSALYA"
Hakika sipati picha ya Bw Msalya
Kwa maana wakati anaondoka hapa, ndiyo kwanza nikifikiriwa kama naweza kuanza shule.


No comments:

Post a Comment