Total Pageviews

Thursday, November 12, 2015

SIMULIZI ENDELEVU YA UKOO WA MSALYA



Nilipata zamani zile
Jumatatu Tarehe 8, Machi 2010 kuwapakulia hapa simulizi za ukoo wa Msalya. Simulizi hizo zikitoholewa na Mzee CK.
Mwezi wa Agosti mwaka huu nilirejea huko Nakatuba katika kikao cha ukoo, kilichoendana na kumbukumbu ya takribani mwaka mmoja toka alipotutoka Mzee CK.
Mzee Mwayai aliongoza tena hizi simulizi endelevu akisaidiana na ndugu zake.

..........ungana nami  tena leo kwenye mwendelezo wa simulizi hii ya ukoo wa  MSALYA.........

MSALYA 1895 – 04 Juni 1966.
Msalya kama alivyokuja kujulikana baadae, alipozaliwa aliitwa jina la Babu yake mkubwa Chisaka. Wengi wanalihusisha jina la Msalya na uoaji wa Wake wengi mmoja baada ya mwingine.
Wakeze Msalya ni pamoja na:
Myango: Mama yake Bhajaraki na Manyori
Bhituro: Mama yake Kulwijira na Mwayai
Bhuinda (Nyamusibha): Mama yake Nyanjura
Nyamata: Mama yake Gabhaseki
Kamwanyi (Amefariki 2013): Mama yao na Chausiku, Tabhu na marehemu Daudi
Mwananonga: Mke wake wa mwisho, ambae hawakujaaliwa kupata watoto  mwenyeji wa Tabora.

Msalya kwa upande wa ndugu, alikuwa na kaka yake akiitwa Nyachiriga. Na pia amezaliwa na dada zake Nyabhwangu, Nyalimbe na Nyaswi.
Nyabhwangu ni dada yake Msalya kwa kuzaliwa na mama mmoja, Bi Mkoko. Ingawa pia kwa upande mwingine ni shangazi yake kwa sababu Nyabhwangu Chisaka ni dada yake Maseme (Baba wa Msalya).

Nyalimbe ndiye mama yao  Karyanja (Mrs Mjengwa au Mama Msiba), Nyamumwi (Mama yake Jangu) na Nyanyama (Mrs Maryanyo au Mama Remi).
Nyabhwangu aliwazaa Mnyaga kwa mme wa kwanza, na mme wa pili akawazaa Manoko, Muruguta, na Nyamakale.
Nyamakale ndie mama yao John na Heri Ndaro.

Nyaswi yeye aliwazaa Nyakobhe na Nyangeta.

Ndugu wengine wa Msalya wanaojulika pia kwa upande wa baba ni pamoja na:
Kwesi: Baba yao Mbulawabho(Mama yake Pamba Mfungo), Kwebheta na Makene
Magesa: Baba yake Masua na ndugu zake
Chausi: Baba yake Goodluck



...............tutaendelea .....................

No comments:

Post a Comment