Total Pageviews

Friday, August 22, 2014

BWANA NDIYE MCHUNGAJI WANGU

Zaburi 23

1  Bwana ndiye mchungaji wangu, Sitapungukiwa na kitu.
2  Katika malisho ya majani mabichi hunilaza, Kando ya maji ya utulivu huniongoza.
3  Hunihuisha nafsi yangu; na kuniongoza Katika njia za haki kwa ajili ya jina lake.
4  Naam, nijapopita kati ya bonde la uvuli wa mauti, Sitaogopa mabaya; Kwa maana Wewe upo pamoja nami, Gongo lako na fimbo yako vyanifariji.
5  Waandaa meza mbele yangu, Machoni pa watesi wangu. Umenipaka mafuta kichwani pangu, Na kikombe changu kinafurika.
6  Hakika wema na fadhili zitanifuata Siku zote za maisha yangu; Nami nitakaa nyumbani mwa Bwana milele.

No comments:

Post a Comment