Total Pageviews

Thursday, November 18, 2010

webcam test

IDD EL HAJI

Jana baada ya pilikapilika za sikukuu na mihangaiko ya hapa na pale, tukatoka hadi kule kipunguni kuangalia mizigo ya Marehemu Josia.
Baada ya tafakuri ya kipi kinaweza kwenda Bunda, kipi cha kubaki na kipi kifanyiwe nini. Hatimae tukafikia muafaka.
Katika safari ya kurejea kwetu Kinyerezi, tukasema si vibaya tukapitia Garden ku pass time.
Kwa wale mnaopajua KM Magereza, madhari yake ipo vizuri sana.
Kwa kuwa Ki Nokia changu nilikuwa nacho nikaona si haba nikanyaka japo picha mbili tatu za kumbukumbu.


VIJANA WA ENZI HIZO

Pekua pekua ya jana imenikutanisha na Picha hii.
Enzi za ujana wao.
Mwayai tulikuwa nae, anakumbuka ilipigwa studio moja mjini Mwanza kwenye miaka ya 1958.

Wednesday, November 17, 2010

LEO NI SIKUKUU

Leo ni sikukuu ya IDD EL HAJI,
Lakini leo pia ni
BIRTHDAY
ya mdau
MANYORI BILLY KURWIJIRA MSALYA
Picha hizi nimezipata asubuhi hii baada ya kuwa ameimbiwa
HAPPY BIRTHDAY
kwa kutumia Ki NOKIA changu kule kwetu Kinyerezi.
Naamini na wadau wengine pia mtaungana na wana Kinyerezi kumwimbia leo.
Katika Anniersary hii ya miaka 25
Lakini leo pia katika Kumbukumbu,
Inatimia miaka 25 toka mpendwa wetu
NYAMALELO BETTER KURWIJIRA MSALYA
alipotutoka kule Nkinga, Nzega.
DAIMA TUTAMKUMBUKA

Tuesday, November 9, 2010

BIRTHDAY YA MDAU - LILIAN


Katika pekua pekua yangu, nimekuta Mdau wetu wa Kagoshima keshokutwa anatimiza umri wa miaka kadhaa................................

TUMPE HONGERA ZAKE


Naamini ndugu zetu hawa watatuwakilisha kukuimbia

HAPPY BIRTHDAY OUR DEAR LILIAN


Wednesday, November 3, 2010

TASWIRA ZA UCHAGUZI KINYEREZI

Na hizi nilizinasa katika pita pita yangu hukuhuku kwetu.
Mlingoti mmoja kwa Bendera za wagombea wote.

Nilifanikiwa kuhudhuria ufunguzi wa Kampeni za udiwani kwa Kata ya kwetu Kinyerezi.
Bahati mbaya sikusikia sera zozote zenye kutia matumaini.

ADHA YA FOLENI ZA DAR






Juzi kati nikafanikiwa kupata taswira hizi za Foleni za Dar Salaam, hizi nilipata katika route ya Kinyerezi hadi Msimbazi mission Centre. Inakera umbali wa chini ya km 10 inakulazimu kutumia muda kati ya saa 1 hadi moja na nusu.