Total Pageviews

Thursday, December 14, 2017

MUNGU NDIYE AJUAE!

Kwa muda mrefu sasa yapata mwezi sasa nikipanga kuipeleka Gari service, hasa kwa hisia za kuwa na kasoro kwenye Usukani.
Jana nilisisitiza kwa Mafundi waichukue, na walifanya hivyo asubuhi.
Huko walikoenda,
Gari imechomoka tairi mitaa ya Goba, Pichani. Hakuna majeruhi.
Hakika Mungu Pekee Ajuae.

KAMBI YA VIJANA KIBIDULA

Kibudula, Iringa
Kambi ya Vijana wa Ki Adiventista Wasabato inayoendelea na imewakutanisha vijana kutoka nchi mbali mbali zipatazo 11.
Mafunzo mbali mbali ya Stadi za kazi na Maisha hutolewa.

Monday, December 11, 2017

ANOTHER GRADUU

Yes, 
Kadri unavyosoma na kusonga, ndivyo unakuwa na nafasi nyingi za kufurahia kuhitimu.
Minoo, ndani ya Miezi Mitatu ana "Graduate" tena.
Lakini hii ni ya kumaliza miezi mitatu ya Pre Form One.
Jumamosi, Muhanga Secondary School

WAIJUA KABILA YA VADOMA

 Kabila ya Wa Vadoma, hujulikana pia kama Dema. Hupatikana Mkoa wa Kanyemba, Kaskazini mwa Zimbabwe kwenye wilaya za Urungwe na Sipolilo.
 Watu wa kabila hili wanakabiliwa na hali ya maumbile ijulikanayo kama "Etrodactyly".
Tatizo hili pia hujulikana kama "Miguu ya Mbuni" na huweza kuathiri Mikono na Miguu.Vidole vya kati hukosekana, na vile vya pembeni hukunjika ndani.
 Tatizo la Miguu ya Mbuni hutokea 1 kati ya 90, Lakini kwa Wa Dema ni kubwa kwa sababu wao wanasisitiza kuoana wao kwa wao tu.
Wa Dema ni waumini wa madhehebu yao ya kiasili au kanisa la Waadiventista Wasabato.

Saturday, December 2, 2017

MTAA KWA MTAA

Kinyerezi yetu,
Mengi yanabadilika,
Ili kuenenda na kujionea mabadiliko,
Maulid Day ilikuwa Kinyerezi Mtaa kwa Mtaa,
na Chochoro kwa chochoro.