Total Pageviews

Thursday, March 17, 2016

UTII BILA SHURTI???

Marufuku kutanua.......
Ama kweli mlinda sheria ndiyo mvunja sheria.
Nyerere Road, leo asubuhi

Tuesday, March 15, 2016

AFYA MGOGORO

Kinyerezi dispensary jumatatu.
Amina afya ilisumbua juzi na jana, hivyo kulazimika jana kufika hospitalini kwa vipimo na matibabu.

KELVIN IN DAR

 Dunia kama kijiji, mambo mengi yamerahisishwa. Hatimae Kelvin safari yake imemfikisha kwa mara ya kwanza kabisa katika jiji la D'Salaam. Tofauti na enzi zile Kelvin ameweza kufuata maelekezo na kufika mwenyewe bila kupokelewa na wenyeji wake.
Inanikumbusha nami mwaka 1980 nilipoingia jijini kwa mara ya kwanza. Niliposhuka stesheni kwa mara ya kwanza, ile picha niliyokuwa nayo ya jiji ilibadilika kabisa. Ni simulizi ndefu, lakini mimi kwa mwenyeji wangu nilifika kesho yake asubuhi baada ya kuwa nimewasili Dar.
Hakika teknolojia ya mawasiliano imebadilisha mambo mengi.

Wednesday, March 9, 2016

AJALI DAR

Mapema alfajiri leo kumetokea ajali mbaya Barabara ya Mandela, maeneo kati ya Matumbi na Buguruni. Daladala aina ya DCM lifanyalo safari zake Gongo la Mboto na Ubungo limegongana na Lori lililobeba ng'ombe.
Kuna vifo na majeruhi kadhaa.
SOURCE:
Mitandao mbalimbali ya kijamii